Mmiliki wa Mabasi ya HBS Ajiua kwa Kujipiga Risasi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mfanyabiashara na Mmiliki wa mabasi ya HBS, Sultan Hemed amejiua kwa kujipiga risasi asubuhi ya leo Aprili 11, 2018 nyumbani kwake Sikonge mkoani Tabora.



Akithibitisha taarifa hizo mbele ya waandishi wa habari, Kamanda wa polisi mkoa wa Tabora, Wilbroad Mutafungwa amesema kuwa marehemu amejipiga risasi mdomoni na kutokea nyuma ya kichwa.

“Tumepokea taarifa za kifo cha mfanyabiashara ambaye ni mkazi wa wilaya ya Sikonge, ambaye anaitwa Sultan Hemed  mmiliki wa mabasi ya HBS leo asubuhi majira ya saa tatu amejipiga risasi nyumbani kwake. Risasi ambayo imeingilia mdomoni na kutokea nyuma ya kichwani,“amesema Kamanda Mutafungwa.

Hata hivyo, Kamanda Mutafungwa amesema kuwa jeshi la polisi limefika eneo la tukio kufanya uchunguzi ili kubaini chanzo cha tukio hilo na kuahidi kutoa taarifa zaidi baadae.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad