Uhamiaji Inatumika Kisiasa Dhidi ya Abdul Nondo Sio Kosa Kuzaliwa Kigoma –Zitto Kabwe

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Uhamiaji Inatumika Kisiasa Dhidi ya Abdul Nondo Sio Kosa Kuzaliwa Kigoma –Zitto Kabwe
Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe amesema kuwa atampeleka Mwenyekiti wa Mtandao wa wanafunzi(TSNP), Abdul Nondo Uhamiaji ambapo jana alipelekwa katika ofisi hizo kwaajili ya kuhojiwa uraia wake.

Zitto kupitia mitandao yake ya kijamii amesema kuwa Idara ya uhamiaji imekuwa ikitumika kisiasa dhidi ya mwanafunzi huyo na sio kosa hata kidogo Abdul Nondo kuzaliwa Kigoma Ujiji.

Nitampeleka Abdul Nondo Uhamiaji tarehe 20/4/2018 kwa mamlaka yangu kama Mbunge wa Kigoma Mjini ( Jimbo analotoka Abdul na wazazi wake na mababu zake).

Idara ya Uhamiaji inatumika kisiasa dhidi ya mwanafunzi Abdul Nondo, Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania. Sio kosa hata kidogo Abdul kuzaliwa Ujiji Kigoma. Imekuwa tabia ya Serikali kuwapa kesi za uraia watu wanaotoka mikoa ya magharibi hasa Kigoma. Suala la Nondo ni vita dhidi ya Watu wa Kigoma. Tutapambana. Tutampigania Abdul Nondo. Watanzania tusikubali upuuzi huu wa watu wa Uhamiaji na Serikali ya Awamu ya awamu ya Tano kuwafanya raia wa mikoa kama Kigoma kuwa raia wa daraja B
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad