City Wamebeba Ubingwa Lakini United Watapewa Pesa Nyingi Kuliko Wao, Sababu ni hii

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Msimu wa EPL 2017/2018 unakwisha rasmi Jumapili ya jana, na mabingwa wameshapatikana ni Manchestwe City huku pia timu zinazoshuka daraja zimeshajulikana ni Stoke City, Swansea na West Bromich Albion.

Kushinda kwa Manchester City kunamaanisha watapewa £153.2m kutoka PL, pesa hizi ni kutokana na namna ambavyo mechi zao zimerushwa na pia kuna kiasi cha pesa ambacho timu zote za EPL hupewa.

Iko hivi City kama bingwa napewa £39.8m kutoka Epl, lakini pia kuna hii pesa ambayo kila timu wanapewa kiasi sawa(equal share) ambapo huwa ni £82m, pia kuna pesa kutokana na idadi ya mechi zako zilizooneshwa live(haki kutoka Epl) na hii walitakiwa kulipwa £31.5m, jumla ya pesa zote hizi ni £153.2m.

Sasa linapokuja suala la United wao japo wamemaliza nafasi ya pili lakini watapewa pesa kuliko bingwa, United watapokea £153.6 kwanini? Baasi ni hivi United wanapokea kama kawaida equal share ya £82m, wakati City anapokea £39.8m za ubingwa, United wanapokea £37.8m ya mshindi wa pili, lakini United mechi zao ambazo PL walirusha hewani live ni mechi mbili zaidi ya City na hii imewapa £33.9m katika mechi hizo na hapa ndipo walipowaacha City.

Suala hili lipo pia kwa mshindi wa 3 na wa 4, Tottenham amemaliza ligi katika nafasi ya 3 lakini jumla ya pesa ambayo wamevuna ni kiasi cha £148.1m, hii ni pesa ndogo kuliko ambayo Liverpool ambao wamemaliza ligi katika nafasi ya 4 wamevuna, Liverpool wamepata £149.6m na hii ni kutokana na mechi zilizoenda live.

Vilabu vilivyoshuka daraja navyo sii haba kwani wameshuka na fungu kubwa la pesa, Swansea amevuna £100m, West Bromich wakiweka mfukoni kiasi cha £98.5m sawa na mshindi wa mwisho Stoke City na hii imechagizwa sana na hii pesa £82.0m ambayo EPL wamekuwa wakitoa kwa kila timu.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Top Post Ad