AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Joyce amesema kuwa matusi hayo na lugha za kebehi kwake anaona ni jambo la kawaida na ni afadhali kwake lakini sio kuvumilia maumivu aliyokuwa akiyapata kwenye ndoa yake na mumewe Henry Kilewo.
“Nachotaka kusema ni kwamba kwa vile nilichangua hii kazi ya kuwa sauti za wanawake najua gharama zipo, na gharama kubwa kabisa ni kutukanwa lakini sio kwamba mimi sioni hayo matusi nayaona lakini navumilia. Kwahiyo sio kwamba siumii naumia!! na kuna wengine wananikosesha dili za matangazo kwenye kipindi changu kwa kuona nimejiharibia na mambo ya kisiasa.“amesema Joyce Kiria kwenye kipindi chake cha Wanawake Live na kufafanua.
“Pamoja na machungu yote ninayoyapitia ya kutukanwa na kukosa wadhamini kwenye kipindi changu nikilinganisha na maumivu ya kwenye ndoa ni bora nitukanwe na jamii lakini sio kuvumilia ukatili na machungu ya ndoa yangu.“amesema Joyce Kiria.
Mwezi Januari, Joyce Kiria aliutangazia umma kuwa yeye na mumewe hawapo sawa kwenye ndoa yao kwani amekuwa akipigwa na kuachiwa majukumu yote ya kifamilia.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK