AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Yanga ikiwa ugenini katika mchezo wake wa makundi Kombe la Shirikisho ilikutana na kichapo cha mabao 4-0, katika mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa July 5, 1962 nchini Algeria. Kwa matokeo hayo Yanga wanaofundishwa na Mkongomani Zahera Mwinyi wanashika nafasi ya mwisho katika msimamo wa Kundi D.
Akizungumzia juu ya hilo, Akilimali alisema kikosi hicho kinatakiwa kujipanga vilivyo kuona kinapiga hatua na kufika mbele zaidi ya hatua hiyo ya makundi ambayo waliwahi kufika katika msimu wa 2015/16 ambapo walishiriki wakiwa wanafundishwa na Kocha Hans van Der Pluijm.
“Inshaallah Mwenyezi Mungu kama akijalia heri safari hii tunataka tuvuke hapa tulipofikia kama hatukufika nusu fainali basi tufike robo fainali na hilo ndilo lengo letu, Wanayanga tutazame tujipange sawasawa, kuhakikisha tunafika hatua hiyo,” alisema Akilimali.
Baada ya mchezo huo na USM Alger, kikosi hicho ya Yanga kinatarajia kujitupa tena uwanjani Mei 16, kucheza na Rayon Sport ya Rwanda katika mchezo wa pili hatua ya makundi ambao utapigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK