AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Moja ya kipengele hicho ni kile cha mwanafunzi ambaye ana mzazi au mlezi ayemiliki biashara au kampuni inayotambulika na mamlaka za usajili, kutoruhusiwa kuomba mkopo.
Akizungumza leo Jumanne Mei 22, 2018 Mkuu wa Idara ya Haki ya Wanafunzi wa mtandao huo, Gibson Eliaform amesema, “Meneja ni cheo tu hakitambulishi uwezo wa mtu hata mwenye kibanda cha huduma za fedha kwa mitandao ya simu na kampuni ndogo iliyosajiliwa anaweza kuwa meneja wa biashara.”
“Anaweza kuwa amesajili biashara yake Brela (Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni ) au TRA (Mamlaka ya Mapato Tanzania) na ana mtaji wa Sh500,000 je huyu ni tajiri?” amehoji.
Amesema kipengele kingine ni kinachozuia wanafunzi waliotajwa katika sheria ya utumishi wa umma kutoomba mikopo, ikiwamo madiwani, maofisa watendaji wa kata na mtaa ambapo kimsingi kazi yao haina mshahara.
Eliaform amesema kigezo hicho hakipo kisheria na huenda kimewekwa makusudi ili kupunguza wanufaika wa mikopo kulingana na bajeti.
Amesema kipengele kingine kinachotakiwa kufanyia marekebisho ni kuzuiwa wanafunzi waliosoma shule binafsi, kubainisha kusoma shule binafsi siyo kigezo kinachotambulisha uwezo wa mzazi kuhimili gharama za masomo Chuo Kikuu.
“Hali hubadilika kuna kufilisika, magonjwa na pia wanaolipa ada ndogo chini ya Sh1 milioni kuwanyima mikopo ni kukatisha ndoto zao,” amesema.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK