Watanzania 11 Waishio Afrika Kusini Walioshtakiwa na Kosa la Ubakaji Waachiwa Huru

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Watanzania 11 Waishio Afrika Kusini Walioshtakiwa na Kosa la Ubakaji Waachiwa Huru
Vijana 11 raia wa Tanzania waishio Johannesburg, Afrika Kusini walioshtakiwa kosa la ubakaji wameachiliwa huru na hakimu mkazi wa Mahakama ya Johannesburg.

Walikuwa wameshtakiwa kwa makosa ya kumteka nyara na kumbaka mwanamke mjamzito Thelma Mondowa raia wa Zimbabwe mwaka uliopita.

Waliachiliwa huru na Jaji Metisie kwa kukosekana kwa ushahidi.

Wakili wa upande wa mashtaka wa serikali alikuwa amemfahamisha hakimu kuwa Bi Thelma Mondowa aliamua kurejea Zimbabwe na wameshindwa kupata anwani yake.

Mwanamke huyo iliarifiwa alikuwa akitoka kazini na mfanyakazi mwenzake wa kiume pale ghafla walipovamiwa na kundi la wanaume wenye silaha na wakamvuta mwanamke huyo kabla ya kumpiga mfanyakazi mwenzake ambae baadaye alifanikiwa kutoroka.

Kisa hicho kilitokea mnamo 15 Mei mwaka 2015 katika barabara ya 270 Lilian Ngoyi mjini Johannesburg.

Washtakiwa wakiwa kortini
Baada ya mfanyakazi huyo kutoroka aliwapigia simu polisi na wakafanikiwa kufika eneo la tukio na kuwakuta wanaume hao wakimbaka kwa zamu mwanamke huyo.

Polisi wapatao kumi waliingia kwenye jengo ambapo tukio lilidaiwa kufanyika na kumuokoa mwanamke huyo na kumpeleka hospitalini.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad