AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Watu watatu wanaotuhumiwa kuwa majambazi wamepigwa mawe hadi kufa na wananchi wa Kijiji cha Bubare Wilaya ya Missenyi mkoani Kagera.
Watuhumiwa hao waliuawa baada ya kuwekewa mtego kutokana na kuwapo taarifa za wao kutaka kuvamia nyumba ya mmoja wa wakazi wa kijiji hicho kwa nia ya kupora fedha za mauzo ya mifugo.
Baadhi ya viongozi wa Serikali ya kijiji waliojaribu kuwazuia wananchi kuwashambulia watuhumiwa hao, walilazimika kutimua mbio kuokoa maisha yao baada ya kugeuziwa kibao na kuanza kushambuliwa.
Mkuu wa Wilaya ya Missenyi, Denis Mwila alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataka wananchi kuacha kujichukulia sheria mikononi wanapowakamata watuhumiwa, badala yake wawafikishe kwenye mikono ya vyombo vya dola kwa hatua za kisheria.
Akizungumzia namna njama za watuhumiwa hao zilivyojulikana na kuwanasa, Mkuu huyo wa wilaya alisema uongozi wa kijiji na jeshi la polisi walipata taarifa kutoka kwa raia wema kuhusu watu kutaka kuvamia nyumba ya mkazi huyo aliyeuza mifugo yake Mei 16. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Augustine Ollomi alisema uchunguzi kuhusu tukio hilo unaendelea na kuahidi kutoa taarifa baadaye
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK