Fedha Yavunja Ndoa ya Mchekeshaji Kansiime Mwenye Afunguka A-Z

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Fedha Yavunja Ndoa ya Mchekeshaji Kansiime Mwenye Afunguka A-Z
Sababu nyingi zimeelezwa kuwa chanzo cha kuvunjika kwa ndoa ya mchekeshaji maarufu Afrika Mashariki, Anne Kansiime na aliyekuwa mumewe Gerald Ojok.

Wapo waliosema fedha, kushindwa kubeba ujauzito au kuchepuka. Tetesi hazijawahi kuacha kusikika kila kona, lakini mwenyewe ameibuka na kukata mzizi wa fitina.

Katika mahojiano yake mwishoni mwa wiki iliyopita, Kansiime alifunguka kwanza kukiri kuvunjika kwa ndoa hiyo akisema anatangaza nafasi kwa mwanamume aliye tayari kuwa naye.

Mtangazaji alipomuuliza sababu ya kuvunjika kwa ndoa yake alisema hana uhakika ila anahisi suala la kipato linaweza kuwa limechangia.

“Mimi nilikuwa naingiza fedha nyingi kuliko yeye, huenda hiyo ni sababu lakini sina uhakika,” anasema.

Katika mahojiano hayo pia alitoboa kuwa ndoa yake ilivunjika muda mrefu lakini alikuwa akiogopa kuwaambia mashabiki wake na watu wa karibu akihofia kuonekana mwanamke mpumbavu.

“Kusema ukweli ndoa yangu ilivunjika miezi sita kabla dunia nzima haijajua. Nilificha nikijipa muda wa kutafakari namna nzuri ya kuwaeleza mashabiki wangu. Niligundua kuwa najiumiza bure kwa sababu sasa nipo huru,” alisema.

Kansiime ni mchekeshaji ambaye amejizolea umaarufu mkubwa Afrika Mashariki kwa uwezo wake wa kuweka utani kwenye maisha ya kawaida.

Pia alijipatia umaarufu kupitia mitandao ya kijamiii ambako alianza kwa kuweka vipande vya video akiigiza kama mwanamke wa Kiafrika anayekutana na changamoto mbalimbali za maisha.

Mchekeshaji huyo wa kike, ambaye pia huendesha kipindi cha “Don’t Mess With Kansiime” kwenye kituo cha Citizen TV, anatajwa kuwa mwanamke mwenye kipaji cha pekee nchini Uganda na Afrika Mashariki kwa ujumla.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Top Post Ad