Serikali ya Rwanda na Arsenal Kufanyiwa Uchunguzi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Serikali ya Rwanda na Arsenal  Kufanyiwa Uchunguzi
Wanasiasa nchini Uholanzi na baadhi ya Wabunge wa Uingereza na Ujerumani, wametaka kufanyika kwa uchunguzi kuhusiana makubaliano ya hivi karibuni yaliyofikiwa na Serikali ya Rwanda kuidhamini klabu ya soka ya Arsenal ya nchini Uingereza.


Uamuzi huo umejitokeza baada ya kuwepo kwa wasiwasi kuhusiana na mkataba huo wa mamilioni wakati mataifa hayo yakitoa msaada mkubwa kwa Rwanda.

Mkataba huo wa udhamini wa miaka mitatu unaojulikana kama Visit Rwanda, unahusu nembo ya Rwanda kuonekana kwenye jezi za timu ya Arsenal ambapo lengo likiwa ni kutangaza vivutio vya utalii vya taifa hilo la Afrika Mashariki.

Wakosoaji wamehoji kwanini serikali ya Rwanda imetumia Paundi za Kiingereza milioni 30 kusaini makubaliano hayo na kudai ni fedha nyingi ambazo zingesaidia kuboresha miundombinu na masuala mengine ya maendeleo na kuhakikisha Wanyarwanda wanajikwamua kutoka kwenye umasikini.

Hata hivyo serikali ya Rwanda imesisitiza kwamba fedha hizo za udhamini zimetokana na mapato ya sekta ya utalii yenyewe na inaamini uamuzi huo utachangia pakubwa kuinua sekta hiyo.

Utalii ndio sekta inayoongoza kwa kuingiza fedha za kigeni nchini Rwanda kiasi cha Dola milioni 400 kwa mwaka ambapo nchi hiyo imepanga kuongeza mapato hayo maradufu na kufikia Dola milioni 800 ifikapo mwaka 2024.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad