Watanzania Waliokamatwa kwa Uvuvi Haramu Kenya Waachiwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Serikali imesema Watanzania 109 waliokamatwa hivi karibuni kwa madai ya kufanya uvuvi haramu Bahari ya Hindi, upande wa Kenya wamepata dhamana na kurejea nchini.

Hata hivyo, bado Serikali za pande zote mbili zinaendelea kufanya mawasiliano jinsi ya kulishughulikia suala hilo.

Wavuvi hao walikamatwa eneo la Shimoni, linalomilikiwa na bandari Kusini Mashariki mwa Kenya karibu na mpaka wa Tanzania na kufikishwa mahakama ya Kaunti ya Kwale mwanzoni wa mwezi huu.

Walizuiliwa baada ya kushindwa kulipa dhamana ya Ksh20,000 (sawa na zaidi ya Tsh 450000) kila mmoja.

Tangu wakati huo Serikali ya Tanzania imesema imeanza harakati za kuhakikisha kuwa raia hao wanaachiwa huru.

Akizungumza na gazeti hili leo Juni 27, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Susan Kolimba amesema raia hao waliachiwa na kurejea nyumbani.

“Tayari waliachiliwa baada ya kupewa dhamana wakati mawasiliano ya kiserikali yakiendelea,” amesema naibu waziri huyo kifupi.

Hata hivyo, hakuwa tayari kutaja tarehe waliyoachiwa  zaidi ya kusisitiza kuwa Serikali inaendelea kujadiliana na Kenya.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Top Post Ad