Amnety Wanataka Malkia wa Urembo Gerezani Kenya Aondolewe Hukumu ya Kifo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Amnety Wanataka Malkia wa Urembo Gerezani Kenya Aondolewe Hukumu ya Kifo
Shirika la Amnesty International limetoa wito wa kubatilishwa kwa hukumu ya kifo iliyotolewa dhidi ya malkia wa urembo gerezani nchini Kenya Ruth Kamande.

Mwanamke huyo alihukumiwa kifo Alhamisi baada ya kupatikana na kosa la kumuua mpenzi wake miaka mitatu iliyopita katika mtaa wa Buruburu, Nairobi.

Bi Kamande, 25, amekuwa akizuiliwa rumande katika gereza kuu la wanawake la Lang'ata jijini Nairobi ambapo mwaka 2016 aliibuka kuwa malkia wa shindano la urembo lililoandaliwa humo gerezani.

Mkurugenzi mkuu wa Amnesty International nchini Kenya Irungu Houghton amesema mwanamke huyo anafaa kusaidiwa kujirekebisha badala kuhukumiwa kifo.

Malkia wa urembo gerezani ahukumiwa kifo Kenya
Hukumu ya kifo dhidi ya Noura Hussein aliyemuua mumewe aliyembaka yafutwa Sudan
"Tunasikitika kwamba Kenya inaendelea kutoa adhabu hii katili, isiyo na utu na iliyopitwa na wakati. Hukumu hii ni pigo kwa rekodi nzuri ya Kenya ya kuendelea kubadilisha hukumu za kifo kuwa hukumu za vifungo jela," amesema.

"Hakuna ushahidi wowote wa kuaminika kwamba hukumu ya kifo huwazuia watu kutekeleza uhalifu zaidi ya adhabu za aina nyingine. Hukumu hii ya kifo inafaa kubatilishwa mara moja na Ruth Kamande asaidiwe kurekebisha tabia."

Ingawa huku ya kifo huendelea kutolewa kwa makosa ya mauaji na wizi wa kutumia mabavu nchini Kenya, haijatekelezwa kwa mfungwa yeyote nchini Kenya katika kipindi cha miaka 30.

Rais Uhuru Kenyatta na mtangulizi wake Mwai Kibaki walibadilisha hukumu ya wafungwa wengi waliokuwa wamehukumiwa kunyongwa katika kipindi cha miaka kumi iliyopita na kuwa vifungo vya maisha jela.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad