Kundi la Waasi la MRDC Latuhumu Kupambana na Jeshi la Rwanda

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kundi la waasi la MRDC latuhumu kupambana na jeshi la Rwanda
Mamlaka nchini Rwanda zimetupilia mbali uvumi kuhusu kuwepo ukosefu wa usalama maeneo yanayozunguka msitu wa Nyungwe, ambapo kundi jipya la waasi wa MRCD linalodai kuwa linataka kuangusha uongozi wa Rais Paul Kageme linasemekana kuwa na ngome yake.

Akiongea na wenyeji wa wilaya wa Nyaruguru, inspekta mkuu wa polisi Emmanuel Gasana alisema kuwa licha ya majambazi wachache kuvuka na kuingia Rwanda na kuwapora watu eneo moja la Nyaruguru hali hiyo ilikuwa imeshughulikiwa vilivyo na vikosi vya usalama na majambazi hao kukimbilia eneo walitoka.

Wanawake wanaotamani kugawanya uongozi
Kundi la MRCD (Rwanda Democratic Movement for Change) limetangaza rasmi uasi dhidi ya serikali ya Rwanda. Msemaji wa kundi hilo meja Callixte Sankara ameiambia BBC kwamba ni mwezi mzima sasa tangu majeshi ya kundi lake yakipigana na majeshi ya Rwanda katika msitu wa Nyungwe kusini mwa nchi hiyo ,na kwamba majeshi yao yamehusika katika mashambulizi ya mwezi uliopita katika kijiji cha Nyabimata karibu na msitu huo.

Ni machache yanayojulikana kuhusu Callixte Sankara, mtu aliyejitangaza kama naibu kamanda na msemaji wa kundi jipya la waasi la Rwanda Movement for Democratic Change.

Kenya, Rwanda zang'ara kwenye viwango vya uvumbuzi duniani
Meja Callixte Sankara, kama avyojitambulisha kwa vyombo vya habari, ni mwanajeshi aliyekuwa mshirika wa karibu wa rais Paul kagame kwenye kundi la Rwanda Patriotic Front (RPF) katika harakati za kupigania ukombozi.

Alikuwa askari mwenye cheo cha chini baada ya RPF kushinda vita vya msituni na kuchukuwa hatamu za uongozi kufuatia baada ya kifo cha rais Juvenal Hybiamamana kwenye shambulzi la ndege.

Haijulikani kwanini Meja Sankara alikosana na utawala wa kagame, lakini alifungwa jela na mahakama ya kijeshi kwa kipindi kisichojulikana kutokana na kile kilichotajwa kama utovu wa nidhamu.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad