Ngoma Akimbilia kwa TB Joshua Kufanyiwa Maombi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Ngoma Akimbilia kwa TB Joshua Kufanyiwa Maombi
IMEELEZWA kuwa, mshambuliaji mpya wa Azam FC, Donald Ngoma raia wa Zimbabwe, wikiendi iliyopita alienda kufanyiwa maombi maalum na mchungaji maarufu nchini Nigeria, Temitope Balogun Joshua ‘TB Joshua’

Katika maombi hayo ambayo yaliyofanyika kwenye kanisa la mchungaji huyo nchini Nigeria na kurushwa na runinga yake ijulikanayo kwa jina la Emmanuel TV, Ngoma alionekana akiombewa kwa kushikwa goti lake la mguu wa kulia ambalo limekuwa likimsumbua kwa muda mrefu.

Tatizo hilo la goti limemfanya Ngoma akae nje ya uwanja kwa muda mrefu na sasa anatarajiwa kurudi uwanjani mwezi ujao na kukosa baadhi ya mechi za mwanzo za msimu ujao wa Ligi Kuu Bara.

Ikumbukwe kuwa, Ngoma aliyejiunga na Azam hivi karibuni akitokea Yanga baada ya mkataba wake kuvunjwa kutokana na matatizo hayo ya goti, alipelekwa Afrika Kusini kufanyiwa matibabu ya kina na hivi karibuni anatarajiwa kurudi uwanjani.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad