Sajenti Aeleza Machungu Aliyonayo kwa Mtoto Patrick

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Sajenti Aeleza Machungu Aliyonayo kwa Mtoto Patrick
STAA wa filamu kutoka Bongo Movie, Husna Idd ‘Sajenti’ ameeleza machungu yake kwa aliyekuwa mtoto wa msanii mwenzake ambaye ni rafiki yake wa karibu, Rose Alphonce, marehemu Patrick na kusema kuwa amemuachia kovu kubwa.



Akizungumza na Ijumaa, Sajenti alisema kuwa, Patrick enzi za uhai wake alikuwa ni rafiki mkubwa wa watoto wake na walikuwa wamezoeana sana hivyo alivyopata taarifa za kifo chake aliumia na hakuamini kwa kile kilichotokea kwa sababu ni mtoto aliyekuwa akimpenda na hata watoto wake walimzoea.



“Nilivyopata taarifa za kifo cha Patrick kwa kweli niliumia sana, nilijaribu kujiangalia nilivyomzoea nikajikuta huzuni kubwa ikinitawala, sikuweza kulala kabisa, kutwa nikilia kwa uchungu kwa sababu tu nilivyokuwa nimemzoea Patrick na hata watoto wangu,” alisema Sajenti.


Akiendelea kuzungumza na Ijumaa Sajenti, alisema kuwa Patrick amemuachia kovu kubwa ambalo haliwezi kupona milele anachofanya sasa hivi ni kumuomba Mungu, ampe subira mpaka atakapompokea mtoto huyo (jana au leo).



“ Hapa namuomba Mungu tu, anipe ujasiri niweze kupata nguvu ya kupokea mwili wake niamini kabisa hayupo nasi maana nina kovu kubwa ambalo haliwezi kukauka kwenye moyo wangu,” alisema Sajenti kwa masikitiko.



Mtoto Patrick alifariki Jumanne iliyopita jijini Nairobi alipokuwa amepelekwa na mama yake huyo kwa ajili ya kufanyiwa matatibu baada ya kugundulika kuwa na uvimbe kwenye ubongo.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad