Trump na Rais wa Urusi Kukutana Leo kwa Mazungumzo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Trump na Rais wa Urusi Kukutana Leo kwa Mazungumzo
Rais wa Marekani Donald Trump na wa Urusi Vladmir Putin muda mchache ujao watakutana kwa mazungumzo, katika makazi ya Rais wa nchi hiyo mjini Helsinki, ambao ni mkutano wao wa kwanza kabisa kuwakutanisha pamoja.

Mpaka sasa hakuna ajenda yoyote ya mkutano huo, ambao utahudhuriwa tu na watafsiri wao.

Aidha licha ya mkutano huo kutotegemewa sana, lakini wanaweza kuonesha dalili mpya za kuanza kwa awamu mpya ya mahusiano kati ya Washngton na Moscow, baada ya kufarakana kufuatia Urusi kuitwaa kwa nguvu Crimea.

Aidha wachunguzi wa mambo wanadhani pia kuna hatua inaweza kupigwa katika kuumaliza mzozo wa Syria na pia mazungumzo kuhusiana na masuala ya Nyuklia.

Mkutano huo unaosubiriwa kwa hamu, unakuja baada ya Warusi 12 kushtakiwa kwa makosa ya kufanya uhalifu wa kimtandao wakati wa uchaguzi wa Marekani wa mwaka 2016.

Rais wa Marekani na mkewe wakiwasili mjini Helisinki, Finland
Awali Rais Trump alisema atalizungumzia suala hilo kwenye mkutano huo, licha ya kwamba mkutano huo hauna ajenda maalumu.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad