DPP Atoa Maelezo Kesi Mke wa Bilionea Msuya

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

DPP atoa maelezo kesi mke wa Bilionea Msuya
MKURUGENZI wa Mashtaka (DPP), amekiri kupokea malalamiko kutoka pande zote mbili katika kesi inayomkabili mke wa marehemu Bilionea Erasto Msuya, Miriam Mrita na mwenzake dhidi ya mauaji ya dada wa bilionea huyo, Aneth Msuya.

Aidha, DPP ameeleza kupitia Wakili wa Serikali Mwandamizi, Patrick Mwita akitoa madai hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.

Mwita alidai kuwa jalada la kesi hiyo lipo mikononi mwa DPP kwa ajili ya utendaji zaidi wa kikazi.

“Mheshimiwa hakimu, DPP amekiri kupokea malalamiko ya pande zote mbili, anaomba mahakama imvumilie wakati analifanyia kazi jalada la kesi hiyo, ili maelekezo atakayotoa yawe ya haki,” alidai Mwita.

Wakili wa utetezi, Peter Kibatala, alidai kuwa hana pingamizi na hoja za Jamhuri na kwamba DPP apewe muda wa kutosha kutenda haki kwa pande zote mbili.

Hakimu alisema upande wa Jamhuri ufuatilie jalada hilo ili mahakama iweze kuendelea na kesi hiyo, Mbali ya Miriam, mshtakiwa mwingine ni mfanyabiashara, Revocatus Muyela.

Katika kesi ya msingi, washtakiwa wanadaiwa kuwa Mei 25, 2016 walimuua kwa makusudi dada wa marehemu Bilionea Erasto Msuya, Aneth Msuya.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad