Kenya Kuanzisha Baraza la Taifa la Kiswahili

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kenya Kuanzisha Baraza la Taifa la Kiswahili
Baraza la Mawaziri nchini Kenya limeidhinisha kubuniwa kwa Baraza la Taifa la Kiswahili ambalo litatwikwa jukumu la kukuza na kuendeleza lugha hiyo nchini humo.

Pendekezo hilo linafuata kipengee 137 cha Mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambacho kinasema kwamba lugha ya Kiswahili itaimarishwa, kukuzwa na kutumika kama lugha ya Jumuiya hii.

Baraza hilo litatumika kutoa ushauri, na vile vile kuimarisha maongozi ya serikali kuhusiana na kukuza, kulinda na kuunga mkono matumizi ya lugha ya Kiswahili na kushirikisha kazi ya mashirika ya kitaifa, kandaa hii, kitamaduni, mashirika ya elimu na mashirika mengine yanayohusika na lugha ya Kiswahili.

Je unazifahamu nchi zinazotumia Kiswahili Afrika?
Kamusi Kuu ya Kiswahili yazinduliwa Tanzania
Wasomi wa Kiswahili na wadau wengine wamekuwa wakihimiza kuundwa kwa baraza hilo kwa muda mrefu.

Prof Hezron Mogambi ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi anasema hatua hiyo ni ya kupongezwa sana.

"Tumekuwa tukiingoja kwa muda mrefu kwa sababu maendeleo na makuzi ya Kiswahili yamekuwa yakikwazwa kwa sababu ya kukosa baraza kama hili. Matumizi sawa ya Kiswahili yamepigwa jeki," amesema.

Kutetea hadhi ya Kiswahili
Miongoni mwa mwengine, anasema baraza hilo litasaidia sana katika kuhakikisha kuwa hadhi ya Kiswahili kama lugha rasmi na ya taifa nchini Kenya na kwamba lugha hiyo "inazingatiwa na kuheshimiwa."

"Kwa sasa hakuna chombo cha kufanya hivyo. Kiswahili kimekuwa kikitumiwa nchini Kenya katika hafla na shughuli mbalimbali kwa njia isiyofaa. Hakuna wa kukosoa na kuelekeza. Matumizi sawa na upotoshaji utazuiwa kwa kuwa na chombo cha kufanya kazi hii," anasema.

Maneno ya Kiswahili yaongezwa kamusi ya Kiingereza
Prof Mogambi anaeleza kuwa kutokana na kutukuwepo kwa baraza hilo, kumekuwa na vitabu vingi ambavyo vimechapishwa kiholela bila kufuata viwango bora vya lugha na vimekuwa changamoto kuu katika kuendeleza lugha ya Kiswahili.

"Hii ni pamoja na vitabu vya shule na vile vya kiada. Uchunguzi na urekebishaji wa maandishi kama haya pamoja na mengine yanaweza tu kurekebishwa na kuhakikishiwa ubora baraza la Kiswahili litakapokuwepo," anasema.

Aidha, anasema baraza hilo litasaidia taaluma ya tafsiri na ukalimani kwa kuwa "kuna matini nyingi sana ikiwemo stakabadhi za serikali, za watu binafsi, mashirika ya ndani ya nchi na ya kimataifa ambazo zahitaji kutafsiriwa. Huduma kama hii itasaidiwa sana na kusawazishwa kimsamiati na barala la Kiswahili."

Mhadhiri na msomi wa lugha ya Kiswahili Hezekiel Gikambi amesema: "Kuanzishwa kwa Baraza la Kiswahili Kenya hata kulikuwa kumechelewa. Tanzania wana Bakita kwa muda Mrefu. Ni hatua nzuri katika kusaidia Kiswahili kukita mizizi kama lugha rasmi nchini Kenya na pia kukidhi hitaji la Jumuiya ya EAC kifungu 137."

"Tunatumai wabunge watagundua hilo wapitishe haraka na wataalamu wa Kiswahili wapate kazi katika Baraza hilo. Kitakuwa chombo rasmi cha kukuza Kiswahili nchini."

Kwa muda mrefu, wasomi wa Kiswahili wamekuwa wakitegemea taasisi na vyama vya Kiswahili ambavyo si za serikali kukusanyika pamoja na kujadili masuala ya lugha.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad