Safari za Nje za Kajala Zazua Gumzo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Safari za Nje za Kajala Zazua Gumzo
SAFARI za nje ya nchi za muigizaji wa sinema za Kibongo, Kajala Masanja zimeibua maswali lukuki huku kila mmoja akisema lake.

Siku za hivi karibuni, Kajala amekuwa akisafiri mara kwa mara kuelekea nchini Dubai hali ambayo imewafanya marafiki zake wahoji anapata wapi jeuri ya pesa wakati kazi yake wanaifahamu.

“Kwa kweli tunashindwa kumuelewa mwenzetu hizi safari zake za kila mara Dubai, anapata wapi hii hela maana kama ni kazi za filamu tunajua sasa hivi soko lilivyo gumu,” alihoji rafiki huyo aliyeomba hifadhi ya jina.

Rafiki huyo alienda mbali zaidi kwa kusema kuwa, mbali na safari hizo, Kajala anatanua sana mjini na inasemekana anashusha bonge la mjengo.

“Kwa kweli mwenzetu sijui ni bwana mpya, sijui ana biashara gani inayomuingizia kipato,” aliongeza rafiki huyo.

Baada ya Ijumaa Wikienda kupata ‘dauti’ hizo kutoka kwa rafiki yake Kajala, lilimtafuta mrembo huyo ambapo alifunguka kuwa kinachompa jeuri ni ubalozi pamoja na kazi yake ya sanaa.

“Wewe unajua mimi ni balozi, pia filamu sijaacha kuigiza iwe ni za watu au za kwangu, mtu anaanzaje kuhoji safari zangu za nje ya nchi?

“Niwashauri wanaoibua hayo maswali kwangu wachape kazi, waache majungu,” alisema Kajala.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad