AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akizungumza na Ijumaa wa Wikienda, Tausi alisema kuwa, Majuto alikuwa baba yake aliyemlea katika maadili mema na aliyetamani sana kumuona anafika mbali kisanaa kwani ndio aliyemfundisha na alikaa naye nyumbani kwake Tanga kwa muda mrefu kama mwanaye wa kumzaa.
“Mimi hapa nalia kwa uchungu mkubwa naumia mno kumpoteza baba yangu aliyenilea katika kazi kwa sababu ni mtu ambaye alikuwa anataka kujua hali yangu kila mara na alipenda mno kuona maendeleo yangu kila siku kama mwanaye,” alisema Tausi.
Akiendelea kuzungumza na gazeti hili kwa uchungu, Tausi alisema kuwa Mzee Majuto hata wakati anakaribia kufariki yeye alikuwa ametoka nje kidogo ya Jiji la Dar lakini alipigiwa simu na dairekta Leah Mwendamseke ‘Lamata’ na kumueleza kwamba anaitwa na Majuto na kweli akawahi kumuona kabla hajakata roho.
“Kama baba angefariki bila mimi kumuona kwa kweli ningeumia sana sana lakini nakumbuka alimwambia dada Lamata, Tausi yuko wapi ndipo aliponipigia simu na kuniambia popote nilipo nirudi nije kumuona baba na kwa bahati mbaya baada ya kumuona pale hospitali kesho yake akafariki,” alisema Tausi huku machozi yakimtoka.
Msanii huyo aliendelea kusema kuwa pamoja na kumpoteza baba yake huyo wa hiari lakini anamshukuru Mungu amemtimizia ndoto yake na ameweza kumtengenezea jina ambalo mpaka sasa anapata kazi mbalimbali za kucheza filamu.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK