AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Rais Kagame amesema hayo wakati akihotubia Bunge nchini humo kwenye mkutano wa kuapishwa kwa wabunge waliochaguliwa hivi karibuni.
Akisita kutaja jina lake amemuonya kiongozi huyo wa upinzani, Victoire Ingabire akisema msamaha alioutoa ndiyo njia aliyochagua ya kuleta amani na kujenga taifa hilo na sio shinikizo kutoka kwa mataifa ya Magharibi.
Kwa upande mwingine, Kagame amewaonya wafungwa wote walioachiwa kwa msamaha wake kuwa wabadilike na kuwa wakimya la sivyo watarudishwa tena jela.
Bi. Victoire Ingabire ni kiongozi wa chama cha FDU, mapema wiki iliyopita baada ya kutoka Jela alimshukuru Rais Kagame kwa msamaha wake, lakini akasisitiza kuwa hakuomba msamaha kwa kuwa hakufanya kosa lolote na kuahidi kuendelea na mapambano yake ya kupigania demokrasia nchini Rwanda.
Bi Ingabire , ambaye ni kutoka kabila la wahutu, alikamatwa na kufungwa baada ya kuhoji ni kwa nini makumbusho ya mauaji ya halaiki nchini Rwanda ya 1994 hayakuhusisha watu wa kabila la Wahutu.
Kwa makosa hayo mwaka 2013 alikutwa na makosa ya uchochezi na kueneza chuki, jambo lililopelekea kufungwa Jela miaka 15.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK