Kocha yanga ajiunga na Singida United

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 Kocha yanga ajiunga na Singida United
Imeelezwa kuwa aliyekuwa Kocha Msaidizi wa Yanga, Shadrack Nsajigwa, amejiunga na timu ya Singida United kwa kusaini mkataba wa miaka miwili.

Nsajigwa amejiunga na walima alizeti hao huku akiendelea kuwa Msaidizi ambapo sasa atakuwa chini ya Mkuu wake, Hemed Morocco.

Kocha huyo amefikiana mwafaka na viongozi wa Singida United tangu aachie ngazi ikiwa ni miezi kadhaa sasa akiwa hana timu.

Ikumbukwe Nsajigwa alieleza kujiondoa Yanga baada ya kuwa na minong'ono kuwa alikuwa akiihujumu timu na kusababisha kupata matokeo mabovu.

Mbali na kuinoa Yanga, Sanjigwa pia aliwahi kuichezea Yanga ambayo ni bingwa mtetezi wa Ligi Kuu Bara mara 27.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad