Sababu za Wanawake Kulia Baada ya Kufanya Mapenzi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Kulia baada ya kushiriki ngono au kufanya mapenzi ni kawaida na hushuhudiwa sana kwa wanawake, ijapokuwa imesemekana kuwa wanaume hulia pia.

Kulingana na wataalam, kuna sababu kadhaa ambazo humfanya mwanamke kulia au kujawa na huzuni baada ya kushiriki ngono, na mojawapo ya sababu hizo ni homoni ambazo mwili wa binadamu hutoa wakati huo. 

Umewahi kushiriki mapenzi na kugundua kuwa mpenzi wako amelia tu, baada ya kipindi kirefu cha kufurahisha?

Kulingana na wanasayansi, ni kawaida.

Utafiti mwingine umeonyesha kuwa kati ya asilimia saba nukta saba na asilimia thelathini na mbili nukta tisa ya wanawake wamewahi kulia baada ya kushiriki mapenzi.


Mtaalam mmoja ameieleza hali hiyo kama 'hali ambayo mwanamke hushindwa kujidhibiti na kulia bila sababu, hasa baada ya kupandwa na raha ya kujamiana, au kufika katika upeo wa raha ya kujamiana 

Umewahi kudhani kuwa 'ustadi' wako ndio uliosababisha kulia kwa mwanamke baada ya kushiriki mapenzi? Pole sana!

Hata hivyo, mtaalam mwingine amesema kuwa ukweli wa mambo na mawazo yanayokuja punde baada ya kushiriki ngono kama woga, huweza kumfanya mwanamke kulia, ijapokuwa amesisitiza kuwa kulia kwa mwanamke baada ya kushiriki mapenzi ni kawaida!
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad