AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mdee amesema hayo katika mahojiano maalum na www.eatv.tv ambapo amefunguka kuwa hakuna diwani wala Mbunge wa CHADEMA ambaye amekwenda kuomba kujiunga na CCM kama Polepole anavyodai.
"Hakuna kiongozi anayeomba kujiunga na CCM, huyu Polepole anatetea kibarua chake tu", amesema Mdee.
Akizungumzia kuhusu viongozi wa upinzani kuhamia CCM amesema kuwa wanasiasa pia ni binadamu na sio malaika hivyo wapo waaminifu na wasiokuwa waaminifu na kinachopelekea yote hayo ni tamaa na ugumu wa maisha.
"Kwenye kazi hii huwezi kukwepa kutofanya kazi na watu wasiokuwa waaminifu na kinachowashinda kukaa upinzani ni uoga hawawezi mapambano wakitishiwa tu kidogo wanahama na sio kwamba wanaomba", amesema Mdee.
Katika mahojiano maalum na www.eatv.tv Septemba 28, 2018 Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Humphrey Polepole alisema kuwa kuna baadhi ya wabunge wa vyama vya upinzani hata wasijisumbue kujiunga na CCM kwani hawatopokelewa na chama hicho na watafute kazi za kufanya ifikapo mwaka 2020 kwakuwa utakuwa ndio mwisho wao kisiasa.
“Kuna wabunge wameshaomba kujiunga na CCM hasa wa Dar es salaam, lakini kutokana na mienendo yao tumewakataa kwani huwezi tukana maendeleo wakati unatumia hivyo hivyo unavyopingana navyo”, amesema Polepole.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK