Nyota wawili wa Azam FC wakosekana miezi miwili

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Nyota wawili wa Azam FC wakosekana miezi miwili
Wachezaji wawili wa klabu ya soka ya Azam FC, kiungo Frank Domayo na mshambuliaji Paul Peter, watakosekana uwanjani kwa takribani miezi miwili, baada ya kugundulika kuwa na matatizo ya goti kila mmoja wakiumia kwa nyakati tofauti.



Kwa mujibu wa msemaji wa klabu hiyo Jaffar Idd, nyota hao wawili watapata matibabu kwa njia tofauti baada ya kupata vipimo nchini Afrika ya kusini.

Jaffar amesema kwa mujibu wa madaktari, Paul Peter amelazimika kubaki nchini Afrika kusini kwaajili ya kufanyiwa upasuaji kutokana na tatizo lake kuwa kubwa na matibabu yake kuhitaji upasuaji tofauti na Domayo ambaye atatibiwa kawaida tu.


''Domayo tumempokea jana Oktoba 15, 2018, kutoka Afrika Kusini na ambapo ripoti ya daktari inasema kuwa hatafanyiwa upasuaji na badala yake atatibiwa hapahapa nchini ila Peter atafanywa upasuaji'', amesema.

Jaffar ameongeza kuwa wanatambua mchango wa wachezaji hao ndani ya kikosi chao na wanawaombea wapone haraka ili warudi kwenye timu kwaajili ya kuendelea na majukumu yao.




----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad