Rais Magufuli Afanya Uteuzi Mwingine Amteua Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi NHC

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Rais Magufuli Afanya Uteuzi Mwingine Amteua Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi NHC
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli amemteua, Dkt Sophia Kongela kuwa Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa NHC.


Awali Dkt Sophia Kongela alikuwa mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Ardhi nchini.

Aidha kupitia Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amemteua Dkt Maulid Banyani kuwa Mkurugenzi Mkuu wa shirika la nyumba la taifa.

Awali Dkt Banyani naye alikuwa mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Ardhi (ARU) nchini ambapo awali nafasi hiyo ilikuwa ikikaimiwa na Felix Maagi

Mapema asubuhi ya leo, Oktoba 30, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli alitangaza kumteua Prof. Humphrey Moshi kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Ushindani nchini (The Fair Competition Commission- FCC).

Tangu aingie madarakani Rais John Pombe Magufuli amekuwa akiwateua wasomi mbalimbali kushika nafasi za uongozi kwenye mashirika ya umma, binafsi na kutoka vyama mbalimbali vya siasa.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad