Kasi ya Kagere Yamuibua Hamissi Tambwe "Kagere ni Moto wa Kuotea Mbali Sitashangaa Akiwa Mchezaji Bora Msimu Huu"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kasi ya Kagere Yamuibua Hamissi Tambwe "Kagere ni Moto wa Kuotea Mbali Sitashangaa Akiwa Mchezaji Bora Msimu Huu"
Mshambuliaji wa Yanga, Amissi Tambwe, ameibuka na kusema straika wa Simba, Meddie Kagere ni moto wa kuotea mbali.

Ni baada ya Kagere kufunga mabao yote mawili juzi, wakati Simba ikiichinja JKT Tanzania 2-0 kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara katika Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

Tambwe amesema amekuwa akimfuatilia kwa karibu mchezaji huyo ambaye alijiunga na Simba Juni, mwaka huu akitokea Gor Mahia ya Kenya.

Tambwe amempongeza Kagere kwa kufikia rekodi yake ya kufunga mabao saba katika mechi 11 za kwanza Simba.



Alisema, yeye pia msimu wa 2013/14 aliposajiliwa na Simba akitokea Vital’O ya Burundi, alifunga mabao saba katika mechi 11 za kwanza.

“Kwa hiyo, Kagere ni mmoja kati ya washambuliaji hatari sana msimu huu na jinsi mambo yanavyoenda, sitashangaa kama ataibuka mfungaji bora.


“Ana tofauti kubwa na washambuliaji wengine wa Simba, anafunga Uwanja wa Taifa lakini pia katika viwanja vya mikoani, kwa hiyo nampongeza kwa hilo, lakini pia kitendo chake cha kuifikia rekodi yangu ya kufunga mabao saba katika mechi 11 za ligi kuu,” alisema Tambwe ambaye msimu huo wa 2013/14 ndiye aliyeibuka mfungaji bora wa ligi kuu baada ya kufunga mabao 19.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad