AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Taarifa za tukio hilo zilizothibitishwa na Mtendaji wa Kata ya Majimaji, Neema Mahujilo, zinaeleza kuwa, radi hiyo iliambatana na mvua kubwa ya upepo iliyonyesha Desemba 14, saa 12. 30 hadi saa 1.40 jioni.
Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Jemini Mushy, alithibitisha kuwapo kwa tukio hilo na kwamba Polisi inaendelea na uchunguzi ili kubaini chanzo cha vifo hivyo.
Kamanda Mushy aliwataja watu waliopoteza maisha kuwa ni Zenna Hamadi Ismail (50), Yusuph Abdalah Alli (25) na Zamila Abdalah Abbilahi (3).
Mganga Msaidizi wa Hospitali ya Wilaya ya Tunduru, Edger Ngauje, aliyeifanyia uchunguzi miili ya marehemu, alisema kuwa chanzo cha vifo hivyo ni kuunguzwa na shoti ya umeme uliosababishwa na radi hiyo.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK