AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kubenea ameyasema hayo jana ikiwa ni siku moja kupita tangu Rais John Pombe Magufuli alipotamka hadharani kuwa wahanga waliobomolewa nyumba kuanzia maeneo ya Ubungo hawatalipwa fidia kwa kuwa walivunja sheria kwa kujenga kwenye hifadhi ya barabara.
Akizungumza jana na wanahabari, Kubenea amedai kushangazwa na kauli ya rais kwamba waliovunjiwa nyumba walijenga kwenye hifadhi ya barabara lakini serikali ndiyo iliyokuwa ikipokea kodi zao, kuwapatia hati za maeneo, kuwawekea maji na umeme huku wakijua hilo ni eneo la hifadhi.
"Naomba wananchi wa Ubungo, Kimara waliovunjiwa nyumba zao wahifadhi vizuri nyaraka zao. Mungu akipenda Sisi CHADEMA tukiingia madarakani tutalipa waathirika wote waliobomolewa kuanzia ubungo hadi Kibaha. Inawezekana siyo lazima CHADEMA waingie madarakani lakini anaweza akaja kiongozi mwingine akalipa. Hii inawezekana," alisema Kubenea.
Akiipigilia msumari kauli yake, Kubenea alisema kwamba, "Jumuiya ya Afrika Mashariki ilivunjika 1977, Serikali ya Mwl. Nyerere haikuipa kipaumbele kuwalipa wastaafu na hata seriakali ya Rais Mwinyi, ila serikali ya Mkapa yenyewe ililipa ikiwa ni baada ya miaka 30. Hivyo wanaweza wasipate wao malipo hayo lakini vizazi vyao vitakuja kunufaika ndiyo maana zipo nchi sasa zinalipwa fidia kutokana na vita vya dunia".
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK