AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mshambuliaji wa Simba, Meddie Kagere ndiye aliyekuwa wa kwanza kufungua kalamu ya magoli katika mchezo huo kwa kuiandikia goli la kwanza timu yake ya Simba mnamo dakika za Nyongeza kipindi cha kwanza na kuifanya Simba sc kwenda mapumziko ikiwa inaongoza.
Kipindi cha pili Bandari waliweza kupata bao dakika ya 59 kupitia penalti iliyopigwa na William Waydi hiyo ilitokana na Mzamiru Yassin kufanya madhambi katika eneo la hatari na alitolewa nje ya uwanja baada ya kuumia na nafasi yake kuchukuliwa na Jonas Mkude.
Bandari waliendelea kulisakama lango la Simba huku wakijilinda zaidi na mnamo dakika ya 75 waliweza kupata goli la 2 na laushindi.
Kwa matokeo hayoBandari inakuwa Timu ya Kwanza kukata tiketi ya kuingia Fainali za Sportpesa huku Timu ya Simba SC inasubiri kucheza mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu dhidi ya Mbao/Kariobang Sharks.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK