AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mshambuliaji wa klabu ya Juventus, Cristiano Ronaldo amepata nafasi ya kumualika mwanamke mmoja shabiki wa timu hiyo aliyejikuta akiingia kwenye matatizo baada ya kumpiga na mpira kwenye paji la uso.
Elene Di Martino alijikuta akitokwa na damu sehemu za pua baada ya kupata majeraha kutokana na shuti kali lililopigwa na Mreno huyo huku mawani yake ya kivunjika wakati Juventus ikikabiliana na Chievo Verona mwanzoni mwa mwezi huu.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 33, alifanikiwa kuiyonga Juventus kuibuka na ushindi wa jumla ya mabao 3 – 0 katika dimba la Allianz.
Mama huyo, Di Martino akiwa chini ya uangalizi wa madaktari akipatiwa matibabu alialikwa na Ronaldo wakati wa mazoezi ya timu hiyo na kupewa jezi iliyokuwa na saini ya Mreno huyo pamoja na kupata nafasi ya kupiga naye picha huku pua yake ikionekana kuwa na bandeji.
Mara baada ya tukio hilo mama huyo aliandika kwenye akaunti zake za kijami kuwa Cristiano ni mfano wa kuigwa kwa upande wake na mara baada ya kupa kipigo hicho alitarajia angealikwa kwenye chakula cha usiku.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK