R. Kelly ageuka dhahabu nchini Ujerumani, Mapromota walazimika kubadilisha ukumbi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Licha ya kuandamwa na tuhuma za unyanyasaji kingono wanawake nchini Marekani, Msanii nguli wa muziki wa R’n’B nchini humo, R. Kelly ameendelea kuwavutia mashabiki wake duniani kote ikiwemo nchini Ujerumani.

Kwa mujibu wa mtandao wa habari za burudani wa Veltra, umeripoti kuwa R. Kelly atatumbuiza mjini Ludwigsburg nchini Ujerumani mwezi April 12, 2019. Hii ni baada ya kubadilisha ukumbi mara mbili kutokana na uhitaji wa tiketi kuongezeka.

Awali R. Kelly alipangiwa kutumbuiza katika ukumbi wa MHP Arena unaochukua watu 7,200, uliopo mjini humo lakini baadae mapromota wakabadilisha ukumbi wa show hiyo na sasa itafanyika katika ukumbi wa
Ratiopharm Arena unaochukua watu 9,000 .


Ratiopharm Arena


MHP Arena

Mtandao huo umeripoti kuwa, tayari tiketi zote 9,000 zimeshanunuliwa tangu watangaze show hiyo mwezi uliopita.

Hata hivyo, waandaaji wa show hiyo wamesema kuwa tarehe ya show inaweza ikasogezwa au watu kurudishiwa hela zao endapo R. Kelly atakutwa na hatia ya unyanyasaji wa kingono dhidi ya wanawake.

Kwa sasa R. Kelly yupo chini ya uchunguzi na mamlaka za usalama za mjini Fulton, Georgia nchini Marekani, kuhusu tuhuma za unyanyasaji wanawake kingono.

Tayari Makampuni na wasanii waliowahi kufanya kazi na R. Kelly nchini Marekani, wamefuta nyimbo mitandaoni. Hii ni kutokana na tuhuma hizo zinazomkumba msanii huyo nguli wa muziki wa R’n’B duniani.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad