AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kwa matokeo hayo Gabon inayoongozwa na Aubameyang imetupwa nje ya michuano hiyo, inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi mwezi Juni mwaka huu nchini Misri.
Mpaka sasa ni mataifa 19 yamefuzu michuano hiyo, huku mataifa mengine matano yakisubiriwa kufuzu leo ili kukamilisha timu 24 zitakazoenda Misri kwenye michuano hiyo.
Leo Tanzania inatupa karata yake ya mwisho kwenye nafasi ya kuwania kufuzu dhidi ya Uganda, ambapo itahitaji matokeo ya ushindi kwanza na baadae waombee Cape Verde waifunge Lesotho au mchezo huo kati ya Lesotho na Cape Verde utoke droo.
Kwa hiyo Taifa Stars hata ikishinda dhidi ya Uganda, halafu Lesotho nayo ikashinda basi tutakuwa tumetolewa kwani Lesotho atakuwa na pointi 8 na Tanzania pointi 8 ila rekodi ya Head to Head, Taifa Stars imepigwa zaidi na Lesotho.
Taifa Stars iliruhusu sae hapa Tanzania na kukubali kichapo nchini Lesotho, hivyo leo Watanzania wanatakiwa waiombee Cape Verde ishinde dhidi ya Lesotho na Taifa Stars ishinde dhidi ya Uganda.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK