RC Makonda Atoa Agizo kwa Viongozi Wilaya za Dar es Salaam

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

RC Makonda atoa agizo kwa viongozi wilaya za Dar es Salaam
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda  ameagiza viongozi wa wilaya za Dar es Salaam kuhakikisha mikataba ya miradi ya kimkakati inasainiwa na ujenzi uanze haraka iwezekanavyo.

Makonda amehoji sababu za fedha kuachwa benki bila kazi kufanyika. Ilala kuna mradi wa machinjio ya Vingunguti na Kinondoni mradi wa fukwe ya Coco.

Aidha Makonda amewaonya wakuu wa Idara zote wanaosimamia Miradi ya Kimkakati kuhakikisha inamalizika katika muda uliopangwa lakini pia wanazingatia viwango Kinyume chake wajiondoe wenyewe katika nafasi zao.

Miezi michache iliyopita Rais John Pombe Magufuri akiwa katika Uzinduzi wa ujenzi wa barabara za njia nane katika eneo la kimara jijini Dar es Salaam alishangazwa na baadhi ya Manispaa kushindwa kutekeleza miradi ya kimkakati ambayo serikali ilishatoa fedha muda mrefu kwa ajili ya Utekelezaji wake.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad