Waziri Mwakyembe Aomboleza Kifo Cha Mtangazaji Ephraim Kibonde

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Waziri Mwakyembe Aomboleza Kifo Cha Mtangazaji Ephraim Kibonde
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison G. Mwakyembe (Mb) amepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Mtangazaji Mahiri wa Clouds Media Group, Bw. Ephraim Samson Kibonde kilichotokea jana Jijini Mwanza.

“Msiba huu ni pigo kubwa  kwetu wanatasnia wa habari nchini, tupo pamoja na  wenzetu wa Clouds Media Group katika kipindi hiki kigumu cha majonzi” amesema Dkt. Mwakyembe.

Enzi za uhai wake Marehemu Kibonde alikuwa Mtangazaji wa Redio ya Clouds Fm katika kipindi cha Jahazi, pia alijihusisha na shughuli ambalimbali za kijamii zikiwemo uandaaji wa  vipindi vya kuelimisha Umma katika masuala ya Makazi na Afya.

Dkt. Mwakyembe ametoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki, uongozi na wafanyakazi wote wa Clouds Media Group pamoja na wadau wa habari nchini.

Imetolewa na

Lorietha Laurence
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,
Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

08/03/2019
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad