"Hatutaki Viongozi Mzigo Uchaguzi ujao"- Polepole

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole, amesema kuwa kuwa viongozi ambao hawafanyi vizuri katika majukumu yao hawatopata ridhaa ya kugombea uchaguzi ujao.


Polepole ametoa kauli hiyo leo Aprili 11, akiwa katika ziara ya kikazi wilayani Ubungo jijini Dar es salaam, ambapo anafuatilia utekelezaji wa miradi kwa mujibu wa Ilani ya chama tawala.

"Lazima mfahamu kuwa wenyeviti wa serikali za mitaa ambao hawafanyi kazi vizuri kwa mujibu wa sheria, hatutawapa nafasi tena katika uchaguzi huu wa 2019", amesema Polepole.

Akizungumzia watumishi wa umma wasio ifahamu ilani ya chama tawala amesema kuwa, "huwezi kuwa unafanyakazi msikitini halafu hujui hata kutamka Asallamu Alleikum, haiwezekani mtu anafanyakazi ya Serikali ya CCM na hataki kuijua Ilani ya CCM, sera zake na taratibu zake".

Sanjari na hayo Polepole amedai kuwa moja kati ya sehemu ambayo CCM inaitazama kwa macho manne ni pamoja na Ubungo, hivyo ni lazima kuimarisha chama katika eneo hilo.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad