Katibu Mkuu CHADEMA atakiwa kwenda kujieleza Mahakamani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imemtaka Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Vicent Mashinji kwenda kujieleza mahakamani kwanini ameshindwa kuhudhuria kesi yake iliyopo mahakamani hapo. 


Dkt. Mashinji ambaye ni mshtakiwa wa sita katika kesi ya kufanya mkusanyiko usiohalali, inayowakabili yeye na vigogo wenzake tisa wa chama, ameshindwa kufika mahakamani hapo kwa maelezo kuwa yupo kwenye kesi nyingine iliyopo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Songea. 


Dkt. Mashinji ametakiwa kwenda kuieleza mahakama hiyo, April 17, mwaka huu sababu za yeye kushindwa kufika mahakama hapo, wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kuanza kusikiliza ushahidi wa upande wa mashtaka. 


Dkt. Mashinji na wenzake wanakabiliwa na makosa 13 likiwemo la kula njama, ambapo wote wanadaiwa kuwa, February 1 na 16, 2018, Dar es Salaam walikuĺa njama ya kutenda kosa la kufanya mkusanyiko usio halali na kukiuka tamko la kutawanyika.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad