Waziri Mbarawa Amtumbua Kigogo Mwingine Wizara Ya Maji

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Waziri Mbarawa Amtumbua Kigogo Mwingine Wizara Ya Maji
Waziri wa Maji Mhe. Profesa Makame Mbarawa (Mb) amemteua Mhandisi Rejea Samweli Ng’ondya kuwa Kaimu Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mjini Mtwara (MTUWASA).

Uteuzi huo ulianza jana Tarehe 12.04.2019. Mhandisi Rejea Samweli Ng’ondya kabla ya uteuzi alikua Meneja wa Mamlaka ya Maji ya Makonde, Mtwara.

Katika hatua nyingine, Waziri wa Maji Mhe. Profesa Makame Mbarawa (Mb) amemteua Mhandisi Charles Richard Mafie kuwa Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira, Wizara ya Maji kuanzia jana tarehe 12.04.2019.

Kabla ya uteuzi huo, Mhandisi Mafie alikua Mkuu wa Idara ya Rasilimali za Maji na Uhandisi wa Umwagiliaji katika Chuo cha Maji – Dar es salaam.

Kufuatia uteuzi huo, Waziri Prof. Mbarawa ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira, Wizara ya Maji Mhandisi Catherine Bamwenzaki kuanzia jana tarehe 12.04.2019

Mhandisi Bamwenzaki atapangiwa majukumu mengine.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad