Sudan Yapigwa Marufuku na Muungano wa Afrika AU

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Tume ya amani na usalama katika muungano huo inasema kuwa ilichukua uamuzi huo kufuatia mauaji ya raia wasio na hatia nchini Sudan katika kipindi cha siku tatu zilizopita.

Muungano huo umetaka uchunguzi kufanywa kuhusu mauaji hayo ambayo yanadaiwa kutekelezwa na vikosi vya usalama.

Tume hiyo inasema kuwa marufuku hiyo ilikubaliwa na wanachama na itaanza kutekelezwa mara moja.

Vilevile imetishia kuchukua hatua dhidi ya watu binafsi katika baraza hilo la mpito iwapo jeshi litakataa kukabidhi mamlaka kwa raia.

Maamuzi hayo yaliafikiwa baada ya kikao cha dharura kilichofanyika kwa takriban saa tano.

Hatua hiyo inajiri huku waziri wa afya nchini Sudan akisema kuwa ni watu 46 pekee waliofariki katika ghasia za hivi majuzi madai yanayopingwa na kamati ya madaktari nchini humo ambao wamesema kuwa idadi hiyo inafika watu zaidi ya 100.

Hali ya wasiwasi imepanda nchini humo tangu Jumatatu wakati ambapo vikosi vya usalama vilianzisha msako dhidi ya waandamanaji wanaounga mkono demokrasia.

Kikosi cha kijeshi cha RPS kilichoshutumiwa kwa kutekeleza mauaji hayo kimekuwa kikipiga doria katika mji mkuu wa Khartoum.

Muungano wa Afrika umeipiga marufuku Sudan kushiriki katika shughuli zozote za Muugano huo hadi taifa hilo litakapounda serikali ya mpito inayoongozwa na raia.

Uamuzi huo unajiri baada muungano huo kuwapatia watawala wa kijeshi wa taifa hilo siku 60 kukabidhi mamlaka kwa raia la sivyo wapigwe marufuku.

Onyo hilo lilijiri baada ya utawala wa jeshi nchini humo kupuuza makataa ya awali ya kujiuzulu katika kipindi cha siku 15 kilioafikiwa na AU mnamo tarehe 15 mwezi Aprili.

Baraza la amani na usalama la AU lilisema kuwa lilijutia hatua ya jeshi hilo kushindwa kukabidhi mamlaka kwa utawala wa raia , lakini likaongezea kwamba linawapatia wanajeshi muda wa siku 60 kufanya hivyo.

Muungano huo ulisisitiza kuwa serikali ya kijeshi haitakubalika na matakwa na mahitaji ya taasisi za kidemokrasia na mikakati yake mbali na kuheshimu haki za binaadamu na uhuru wa raia wa Sudan.

Jeshi lilichukua mamalaka nchini Sudan baada ya kumpindua kiongozi wa muda mrefu Omar al Bashir kufuatia miezi kadhaa ya maandamano dhidi ya serikali.

Iliamua kufanya uchaguzi baada ya miaka miwili lakini waandamanaji wamekataa hilo na kusalia katika barabara za mji mkuu wa Khartoum , wakitaka utawala wa kiraia mara moja.

Baraza hilo likiongozwa na jenerali Abdul Fattah al-Burhan limekuwa likijadiliana na viongozi wa maandamano kuhusu uundaji wa serikali ya mpito.

Lakini pande hizo mbili zimetofautiana kuhusu jukumu la jeshi ambalo limetawaliwa na wandani wa al-Bashir.

Wakati huohuo Maafisa nchini Sudan kwa mara ya kwanza wamethibitisha kuwa hali siku ya juma wamekanusha madai kuwa watu 100 waliuawa na wanajeshi wakati wa maandamano na kukiri kuwa ni watu 46 waliyouawa katika purukushani hilo.

Madaktari wanaohusishwa na vuguvugu la waandamanaji wanasema idadi ya watu waliouawa na vikosi vya usalama wiki hii imepanda na kufikia zaidi ya watu 100.

Walisema miili 40 iliopolewa kutoka mto Nile mjini Khartoum siku ya Jumanne.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad