AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Rais wa TP Mazembe Moise Katumbi |
RAIS wa TP Mazembe, Moise Katumbi ameruka tuhuma za gazeti moja la Madagascar kwamba alimhonga kipa wa Zimbabwe kwenye mechi ya Afcon kuwania kufuzu 16 Bora dhidi ya DR Congo.
DR Congo ya Mwinyi Zahera ilishinda mabao 4-0 kwenye mchezo huo na kufuzu jambo ambalo liliibua mijadala mingi.
Habari zilimhusisha Katumbi na kipa wa Zimbabwe kwamba amempa mshiko ili alegeze jambo ambalo amelikana na tayari amepeleka utetezi wake Caf.
Kupitia ujumbe wake kwenye Twitter yake, Katumbi amesisitiza madai hayo ni ya hovyo na kwamba hata siku mechi hiyo inachezwa hakuwepo Misri alisharudi zake Congo.
Kiongozi huyo mwenye heshima kwenye soka la Afrika amesisitiza kwamba hawezi kuhusika kwenye mambo ya hovyo kama hayo ya kupanga matokeo. Huku uchunguzi ukiendelea, DR Congo itacheza na Madagascar leo Jumapili kwenye mechi ya 16 Bora
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK