Askari Nane Wafutiwa Kesi yao ya Kusindikiza Shehena ya Dhahabu Kutoroshwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Askari nane wa jeshi la polisi ambao walishtakiwa kwa kosa la kusindikiza shehena ya dhahabu imefutwa na taratibu za kuwarejesha kazini tayari zimeanza.

Kadhalika, zimefutwa kesi 70 zilizokuwa kwenye gereza kuu la Butimba baada ya Rais John Magufuli kutembelea gereza hilo mkoani huko.

Askari hao walifunguliwa kesi namba moja ya uhujumu uchumi ya mwaka 2019 katika Mahakama ya Mwanza.

Waliofutiwa kesi hiyo ni Mkuu wa Oparesheni mkoa wa Mwanza, Morice Okinda, E 6948 D/CPL Kasala, F 133 PL Matete, G 6885D/C Alex, G 5080 D/C Maingu, G 7244D/C Timothy, G 1876 D/C Japhet na H 4060 DC David Kadama.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP), Biswalo Mganga, akati akizungumza na waandishi wa habari kuwa ameifuta kesi hiyo kutokana na maslahi ya Taifa.

“Nieifuata kesi hiyo kutokana na kwamba ina mambo mengi yanayohusu maslahi ya taifa ila kuna kesi nyingine inayohusu dhahabu na watuhumiwa wawili watafutiwa kesi hiyo na wengine wataendelea,” alisema.

Awali askari hao walifikishwa katika Mahakama ya Mwanza Januari 11 mwaka 2019 pamoja na wafanyabiashara wane wakikabiliwa na makosa matano ya kutakatisha fedha, uhujumu uchumi na kula njama ya kupanga uhalifu.
Makosa hayo wanadaiwa kuyatenda kati ya Januari 4 na 5 mwaka huu.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad