AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Dk. Bashiru ameyasema hayo wakati akitoa pongezi kwa hatua ya wanaCCM Mkoa wa Dodoma, kutaka Kanali Abdulrahman Kinana na Yusuf Makamba, makatibu wastaafu wa CCM kuchukuliwa hatua.
Makatibu hao wastaafu wiki iliyopita, walimwandikia barua Pius Msekwa, Katibu wa Baraza la Viongozi Wastaafu wa CCM wakilalamikia kuchafuliwa na Cyprian Musiba, anayejitambulisha kuwa mtetezi wa Rais John Magufuli.
Kwenye barua hiyo, Makamba na Kinana wamelalamika kuchafuliwa na kuzushiwa huku wakidai serikali imeshindwa kuchukua hatua na kuhoji ulinzi ulinzi anaopewa mtu huyo anayewachafua.
“Wapuuzeni, hatuogopi kukosolewa, lakini hatuko tayari kudharauliwa, kutukanwa na kubezwa na majina yaliyo na kebehi na watu wasio na shukrani, hatujafunzwa hivyo, hatujazoea hivyo,” amesema Dkt. Bashiru
Aidha, amesema kuwa uongozi wa CCM hautaruhusu malumbano ndani ya chama hicho, huku akieleza kwamba mwenyekiti wake, Dkt. Magufuli yuko tayari kuwasamehe, ili kukijenga chama.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK