Emirates Kurejesha Safari Zake Sudan

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Emirates Kurejesha Safari Zake Sudan
Shirika kubwa kabisa la ndege katika Mashariki ya Kati, Emirates Airline, limesema leo kuwa limeamua kuanzisha tena safari kwenda Sudan kuanzia Julai 8 baada ya kusitisha kwa mwezi mmoja kutokana na machafuko yaliyosababisha umwagikaji damu.

Taarifa ya Emirates imesema kuwa wamechukua uamuzi huo baada ya kufuatilia kwa karibu hali nchini Sudan na kutathmini kwa kina mazingira yote ya uendeshaji huduma.

Emirates itakuwa na safari moja ya ndege kila siku nchini Sudan. Viongozi wa maandamano wameingia katika siku ya pili ya mazungumzo na watawala wa kijeshi yakiwa ni ya kwanza ya aina yake kuwahi kufanyika tangu kushambuliwa kwa waandamanaji mwezi uliopita.

Kiongozi mmoja wa waandamanaji, Ahmed al-Rabie amesema kuwa mazungumzo ya leo yanajikita katika suala la nani ataongoza baraza huru la mpito. Mpango wa Ethiopia na Umoja wa Afrika unatoa wito wa kuundwa baraza litakaloongozwa na raia wengi.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad