Mahakama Yakwama kutazama mkanda wa video kesi ya viongozi 9 wa CHADEMA

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imekwama kuangalia video inayowahusu viongozi 9 wa CHADEMA akiwemo Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe kutokana na upande wa utetezi kuipinga.

Pingamizi hilo liliwasilishwa na Wakili wa utetezi, Peter Kibatala baada ya Wakili wa Serikali Mkuu, Paul Kadushi kuiomba mahakama mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu,Thomas Simba kuandaa mazingira wezeshi ya kuonesha maudhui ya video iliyochukuliwa wakati wa kufunga kampeni za uchaguzi mdogo Jimbo la Kinondoni.

Upande wa mashitaka uliomba mahakama hiyo itumie Kituo cha Mafunzo cha Kisutu kuonesha maudhui hayo kwa sababu kina vifaa vinavyowezesha kuonekana kwa video hiyo vizuri.

Hata hivyo, Wakili Kibatala alidai upande wa mashitaka ulipaswa kuandika barua kwa uongozi wa mahakama kuomba kutumika kwa kituo cha mafunzo kuonesha maudhui hayo.

Pia amedai, walipaswa kuandaa vifaa vyote muhimu ikiwemo waya na projekta ambavyo vingewezesha kuonekana kwa video hiyo na sio wajibu wa mahakama kuandaa.

Kutokana na mvutano wa kisheria baina ya pande mbili, Hakimu Simba ameahirisha kesi hiyo hadi August 5, 6 na 7, 2019 kwa ajili ya kutoa uamuzi kama video itizamwe ama lah pamoja na kuisikiliza kesi hiyo.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad