Mwandishi wa Habari mikononi mwa TAKUKURU kwa kuomba rushwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Na John Walter-Manyara

Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Manyara inamshikilia Patrick Michael Chambo mwandishi wa habari wa kujitegemea kwa tuhuma za kuomba Rushwa ya shilingi laki tatu kwenye kiwanda cha Pombe kali Cha Mati Super Brand Ltd mjini Babati.

Inaelezwa kuwa Mtu huyo  aliomba rushwa hiyo kwa kuwatisha wamiliki wa kiwanda hicho kuwa anayo taarifa zinazohusu kiwanda hicho kukwepa kulipa kodi ya serikali hivyo angewaandika vibaya asipopewa kiasi hicho cha pesa.

Mkuu wa Takukuru mkoa wa Manyara Fidelis Kalungura ameiambia Muungwana Blog  kuwa mtuhumiwa huyo aliendelea kufanya mawasiliano kwa njia ya simu na mmoja wa wakurugenzi wa Mati Super Brand Ltd ambapo ilipofika tarehe 2 April mwaka huu alipokea hongo ya shilingi 150,000 kwa  njia ya Mpesa ikiwa ni sehemu ya fedha alizoziomba ili asiziandike taarifa hizo kwenye vyombo anavyo viandikia.

Kwa kuwa TAKUKURU waliendelea kumfuatilia mtu huyo,walifanikiwa kumkamata wilayani Korogwe mkoani Tanga June 28 na kusafirishwa hadi Babati  ambapo baada ya kuhojiwa  alipata dhamana na kutakiwa kurudi July 9 lakini alikiuka masharti ya dhamana hadi alipokamatwa tena July 19 wilayani Hai mkoa wa Kilimanjaro.

Hata hivyo Kalungura ameeleza kuwa mtuhumiwa huyo anashikiliwa na TAKUKURU mkoani hapa na anatarajiwa kupandishwa mahakamani muda wowote taratibu za kisheria zitakapokamilika ili kujibu tuhuma hizo.

Kalungura amewataka waandishi wa habari na wananchi wote wa mkoa wa Manyara wajiepushe na vitendo vya rushwa na kufanya kazi kwa kuzingatia sheria,kanuni na taratibu pamoja na maadili ya kazi zao,vinginevyo watakumbana na mkono wa Sheria.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad