Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda Awashukia ‘Akina Membe’ Wanaotaka Urais

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda amewashukia watu wanaodaiwa kuwa wanataka kuwania nafasi ya kugombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) mwaka 2020.

Akizungumza jana jijini Dodoma katika uzinduzi wa mradi wa vibanda vya biashara vya chama hicho, Pinda alieleza kuwa wanaofanya mchakato huo wanajisumbua na kutapatapa kwani sio utamaduni wa chama.

Kada huyo mwandamizi wa CCM alisema amekuwa akisikia kuna mtu anayetapatapa kuusaka urais 2020 akilenga kumpinga Rais John Magufuli. Alisema kwa jinsi alivyofanya kazi na Serikali za awamu zote nne, anajua jambo hilo haliwezekani.

Aidha, alifafanua kuwa Rais Magufuli anaelekea kumaliza awamu yake ya kwanza na ataendelea na awamu yake ya pili na sio vinginevyo, huku akidai huenda kukawa na minong’ono baada ya awamu ya pili kumtaka aongezewe muda.

Katika kipindi cha hivi karibuni, kumekuwa na mvutano kati ya baadhi ya makada wa chama hicho huku kukiwa na tetesi za aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nchi, Bernard Membe kutaka kuwania nafasi ya kugombea urais 2020.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad