Apigwa Risasi na Kufariki kwa Kumcheleweshea Mteja Sandwich yake

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Muhudumu mmoja wa mgahawa mjini Paris amepigwa risasi hadi kufa na mteja ambaye amedaiwa kwamba alikuwa amekasirishwa kwa kuwa sandiwich yake haikuandaliwa haraka iwezekanavyo.

Maafisa wa polisi wanasema kwamba uchunguzi umeanzishwa baada ya tukio hilo siku ya Ijumaa jioni mashariki mwa eneo la Le-Grand.

Mshukiwa alitoroka katika eneo hilo na hajapatikana.

Wafanyakazi wa ambalensi walijaribu kuokoa maisha ya muhudumu huyo ambaye alikuwa amepigwa risasi katika bega lake lakini alifariki papo hapo.

Wenzake waliambia maafisa wa polisi kwamba mteja huyo alikuwa na hasira katika duka hilo la Pizza na Sandwich kutokana na muda mrefu ambao sandwich hiyo ilichukua kuandaliwa.

Mauaji hayo yamewashangaza wakaazi na wamiliki wa maduka.

'' Inasikitisha'' , mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 29 aliambia chombo kimoja cha habari nchini Ufaransa .

''Ni mgahawa uliotulia sana na hauna matatizo. Ulifunguliwa miezi kadhaa iliopita''.

Baadhi ya wakaazi, hatahivyo wamesema kwamba kumekuwa na ongezeko la visa vya uhalifu katika eneo hilo mbali na ongezeko la visa vya ulanguzi wa mihadarati pamoja na unywaji pombe barabarani
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad