Ataka Wabunge wasipewe fomu 2020, mpaka wapimwe

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Mkoa wa Dar es salaam, Musa Kilakala, amependekeza kupimwa kwa baadhi ya Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kile alichodai kuna baadhi yao


wanajihusisha na matendo yasiyokuwa na maadili ikiwemo kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja.

Musa Kilakala ametoa kauli hiyo wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Tanga Kijani, iliyofanyika mkoani Tanga, ambapo amemuomba Spika Ndugai kama ambavyo Bunge limeazimia kupimwa ulevi kwa Wabunge, pia liwapime Wabunge ambao wanahisiwa wanajihusisha na vitendo hivyo.

"Kuna mkakati mkubwa kuna baadhi ya Wabunge kuna jambo wamekubaliana, na wanataka kutuletea mambo yasiyofaa ndani ya nchi yetu, na lengo lao kubwa ni kutetea mapenzi ya jinsia moja." amesema Kilakala.

"Napendekeza ikifika uchaguzi 2020, lazima kuna baadhi ya Wabunge wapimwe kabla hawajapewa fomu, namuomba Spika Ndugai kama ameweka vipimo, vya kuwapima baadhi ya Wabunge kuhusiana na ulevi pia aanze kuwachunguza wanaotajwa kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja." amesema Kilakala.

Kwa sasa chama hicho kinafanya kampeni ya Kijani kwa ajili ya kujiandaa na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2020.



----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Swadakta....!!!
    utampaje mtu fomu kama Halima / Zitto /Ester/Gauye

    Hawa wamedhihirisha upotovu wa Nidhamu wa hali ya juu..ambayo inabidi tuwapime kabla yaa kupewa fomu.

    ReplyDelete

Top Post Ad