Mashabiki Wamkataa Neymar PSG

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mashabiki Wamkataa Neymar PSG
Mashabiki wa Paris Saint-Germain wamemtolea uvivu mshambuliaji Neymar katika mechi ya ufunguzi wa Ligi Kuu Ufaransa iliyochezwa jana.

Licha ya kupata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Nimes, mashabiki wa PSG walikwenda uwanjani na mabango ya kumtaka Neymar kuondoka ndani ya klabu hiyo.

Neymar ameibua mzozo wa muda mrefu na klabu yake akishinikiza kuondoka katika usajili wa majira ya kiangazi.

Miamba ya soka Hispania Barcelona na Real Madrid, inahusishwa na mpango wa kumsajili nahodha huyo wa zamani wa Brazil.

Mbali na kwenda mabango, mashabiki hao walipaza sauti wakitaka PSG kuharakisha uhamisho wa Neymar kwa kuwa hawamtaki.

Mashabiki wa PSG hawaoni mchango wa Neymar kama Kylian Mbappe, Edinson Cavani na Angel Di Maria ambao wamekuwa wafungaji wa timu hiyo katika mechi za mashindano.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad