DC Aagiza Wachimbaji Madini Kukamatwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

DC Aagiza Wachimbaji Madini Kukamatwa
Mkuu wa Wilaya ya Chato, Mtemi Msafiri, ameamuru kukamatwa kwa wachimbaji wakubwa wa madini katika eneo la Matabe wilayani humo, ambao wanadaiwa kuwa wasumbufu kwa wachimbaji wadogo wa madini katika eneo hilo.


Mkuu wa Wilaya Mtemi ametoa agizo hilo wakati akizungumza na wachimbaji  wadogo zaidi 1000, katika eneo la Matabe, kikao ambacho kilihudhuriwa na Naibu Waziri wa Madini, Constantine Kanyasu, ambapo amesema licha ya maamuzi hayo wachimbaji hao wafuate sheria.

Maamuzi hayo yamekuja kufuatia malalamiko mengi kutoka wachimbaji wadogo kuwalalamikia wachimbaji wakubwa.

"Malalamiko haya yanayotokea kwa wachimbaji hawa wadogo, sisi kama Serikali hatukubali kuyavumilia, OCD nakuagiza hakikisha wachimbaji wakubwa unawakamata na wanachukuliwa hatua za kisheria", amesema Mkuu wa Wilaya Mtemi.

Awali Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu, ameiagiza Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), kupitia Menejimenti ya Shamba la Miti la Biharamulo mkoani Geita, idhibiti upanuzi wa uchimbaji madini unaofanywa na wachimbaji wadogo nje ya yale ambayo yanatambulika kwa shughuli hiyo katika Shamba hilo.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad